Posts

Showing posts from February, 2024

CHAMWINO DC YATAKIWA KUJITAFAKARI

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kukamilisha ujenzi wa uzio wa ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kabla ya tarehe 30/3 / mwaka huu. Maagizo hayo yametolewa Leo Februari 21,2024  baada ya kuonekana kudorola Kwa mradi huo Kwa zaidi ya miezi 8 tangu ulipotakiwa kukamilika  mwezi julai 2023. "picha ya Chamwino Kwa Sasa siyo nzuri, Mkoa una Halmashauri nane na katika Halmashauri hii kila miradi inayokuja lazima zijitokeze changamoto, tunapokea malalamiko yenu mengi  hasa suala la malipo Kwa wakandarasi wanaojenga miradi yenu, Mhe.Rais anatoa fedha zote ila nyie mnachelewesha kuwalipa  na hiyo ndio sababu inachangia mradi kutokukamilika kwa wakati. nitoe maagizo tarehe 30/03/2024 mradi uwe umekamilika kwa ubora wake na ukamilike kwa fedha ambazo zilitolewa  na ikiwezekana fedha zibaki na zifanye kazi nyingine". Ameelekeza Mhe.Senyamule  Aidha Mhe. Senyamule amemsimamisha kazi mtendaji wa kata ya...

SENYAMULE APOKEA MAUA YA UPENDO KWA NIABA YA RAIS

Image
  Ikiwa ni siku ya wapendanao Duniani ambayo huadhimishwa  Kila mwaka Februari 14, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule amepokea maua ya upendo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan. Zawadi hizo zimetolewa na Wadau mbalimbali ambao Wametoka katika Mikoa ya Arusha,mara na Zanzibar huku wakiongozwa na kampeni ya "MAUA YA MAMA". Kikundi hicho kimehusisha  waendesha baiskeli na na boda boda  ambao walianza safari Yao katika Mkoa wa Mara na leo hii wamehitimisha safari Yao katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. #upendokwamama #mauayamamasamia #Dodomafahariyawatanzania #Happyvalentineday

TATHMINI KUFANYIKA BONDE LA MZAKWE, WAKAZI WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO

Image
  Wananchi wanaoishi  maeneo ya karibu na Bonde la Mzakwe wametakiwa kutoa ushirikiano katika zoezi la tathmini linalofanyika na timu ya watalaam ambayo imeundwa kwa ajili ya kupata taarifa sahihi za  maeneo hayo ili kusadia  ushauri na  maamuzi  yatakayotolewa  katika harakati za kunusuru bonde hilo ambalo ndio chanzo kikuu cha Maji kwa Mkoa wa Dodoma. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa  Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule Februari13,2024 wakati akiitambulisha timu hiyo  kwa wananchi wanaoishi maeneo ya Bonde hilo na  maeneo jilani ambapo utambulishi huo umefanyika katika  Ukumbi wa Veyula Jijini Dodoma. "  Kuna timu ya watalaam itapita kwenu kuja kupata taarifa ni watu wanaokuja kwa amani na wakute amani ,watafanyakazi kwenye maeneo yanayozunguka Bonde watapita nyumba kwa nyumba Ili kupata taarifa za Msingi na hiyo kazi kuanzia tarehe 14 hadi  21 Februari ", Amesema Senyamule  Kwa Upande Wake Mkuu wa Wilaya ya Dodoma M...

RC SENYAMULE KUDILI NA WATAKA RUSHWA

Image
Suala la kuongea, kusikiliza na kutatua kero  za makundi mbalimbali ya wakazi wa Jiji la Dodoma wakiwemo wafanyabiashara, madereva boda boda, wachimba madini n.k limekua endelevu kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule na lenye matokeo chanya na muitikio mkubwa kwa makundi husika. Februari 11/2024 katika ukumbi wa New Generation- Kisasa  katika semina ya siku moja ni zamu ya Mafundi Ujenzi wa Mkoa wa Dodoma ambao nao wanapata wasaa wa kuteta na Mhe. Senyamule ambae anawahakikishia kupambana na wote wanaoleta vikwazo mbalimbali ikiwemo kuombwa rushwa pindi wanapoomba kujenga Miradi ya Serikali pale inapotangazwa licha ya kukidhi vigezo muhimu. "Naomba niwahakikishie kuwa tunaendelea kushughulika na wote wasio na dhamira njema na Mhe. Rais ya kutamani nyie mfanye kazi za Ujenzi wa Miradi ya Serikali bila kikwazo pale mnapokidhi vigezo, namba zetu mnazo mkikutana na vikwazo vya rushwa wakati mnaomba kazi tutumieni meseji na sisi tutashughulika nalo kwa haraka sana", a...

SENYAMULE AKEMEA UHARIBIFU WA MLIMA SAUNA-KONDOA

Image
Ikiwa ni muendelezo wa ziara za kikazi za Ukaguzi wa Miradi ya maendeleo, kusikiliza na kutatua kero za wananchi na kukagua na kuhamasisha utunzaji endelevu wa mazingira kwa Halmashauri zote za Mkoa wa Dodoma Mhe. Senyamule amefika Wilayani Kondoa kujionea namna shughuli mbalimbali zinavotekelezwa Wilayani humo. Akiwa Wilayani humo amewataka wananchi wa Kata ya Bereko hususani   Kijiji cha Kisese wanaofanya shughuli za kilimo katika mlima Sauna kupanda miti katika mashamba yao na kuachana na shughuli za kilimo na uchimbaji wa madini  Ujenzi katika mlima huo. Senyamule ametoa maagizo hayo Februari 9/2023 alipofika kujionea  namna ambavyo mlima huo umeathiriwa na shughuli za mbalimbali za kibinadamu. "Suala la kutunza mlima huu tulipe uzito na tusilete lelemama, viongozi wa hapa hakikisheni kila mtu anayelima katika eneo hili anapanda Miti kwenye shamba lake ndani ya wiki mbili ikiwa ni ishara kuwa mwaka huu ni wa mwisho kulima hapa na hatolima tena. Aidha Mhe. Senyamu...
Image
Shirika la Global Communities Tanzania kupitia mradi wa ‘Pamoja Tuwalishe’ unaotekelezwa katika shule 75 za Msingi  kwenye Halmashauri tatu za Mkoa wa Dodoma ambazo ni Mpwapwa, Kondoa na Chemba, wamekabidhi vishikwambi 75 kwa uongozi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kukusanya taarifa na kupata mafunzo mbalimbali ya lishe kwa njia ya kidigitali kwa shule 75 zitakazopatiwa Vifaa hivyo. Pia Mradi huo unatoa ufadhili wa Chakula ( Mchele, Maharage na mafuta ya kupikia ) kwa shule   hizo huku dhamira kuu ikiwa kusaidia kuboresha juhudi za kusoma na kupandisha ufaulu kwa wanafunzi pamoja na kuimarisha afya na lishe bora kwa wanafunzi.   Makabidhiano hayo yamefanyika leo Februari 09, 2024 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuuwa Mkoa Jengo la Mkapa ambapo waliokabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya Global Communities Tanzania ni Kaimu Mkurugenzi Bi. Vicky Macha, Meneja Mwandamizi wa Ufuatiliaji, tathmini na mafunzo Bw. Wilfred Donath na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala...

WAZIRI MCHENGERWA AZINDUA MAJARIBIO YA UFUNDISHAJI MUBASHARA

Image
Wazari wa Nchi ,Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Mohamed Mchengerwa Leo Februari 7,2024 amezindua majaribio ya ufundishaji mubashara (Live Teaching)  katika Shule ya Sekondari ya Dodoma . Akizungumza mara baada ya uzinduzi huo Waziri Mchengerwa ametoa maelekezo kwa Wakuu wa Mkoa na Wakurugenzi wa Halmashauri Nchini kuhakikisha wanateua Shule moja kwa kila Mkoa zitakazotumika kusambaza mfumo huo kwenye maeneo yao "Wakuu wa mikoa pamoja na makatibu tawala wa mikoa wahakikishe kwamba wanateua Shule maalum ambazo zitakuwa nguzo ya kusambaza mifumo hii ya TEHAMA katika Shule mbalimbali kwenye maeneo yao"  Amesema Waziri Mchengerwa  Uzinduo huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali akiwamo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule, Wakuu wa Wilaya na Maafisa elimu