Posts

Showing posts from May, 2025

VITUO VYA ‘KILIMO ANGA’ NCHINI, KUPATA NDEGE MPYA ZA KUDHIBITI VISUMBUFU VYA MIMEA

Image
  Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe,akitoa maelekezo kwa watendaji wa Wizara yake kuhusu kufanyika mchakato wa ununuzi wa Ndege tatu za kudhibiti visumbufu vya mimea wakati wa hafla ya kupokea ndege moja iliyonunuliwa kwa lengo hilo leo Mei 30, 2025 kwenye Kiwanja kidogo cha Ndege Jijini Dodoma. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akiishukuru Wizara kwa ununuzi wa ndege ya kudhibiti visumbufu vya mimea wakati wa hafla ya kupokea ndege moja iliyonunuliwa kwa lengo hilo leo Mei 30, 2025 kwenye Kiwanja kidogo cha Ndege Jijini Dodoma. Waziri wa Kilimo Mhe. Bashe akikagua ndege mpya iliyonunuliwa na Serikali kwa lengo la kudhibiti visumbufu vya mimea wakati wa hafla ya kupokea ndege hiyo iliyofanyika leo Mei 30, 2025 kwenye Kiwanja kidogo cha Ndege Jijini Dodoma. Viongozi wa dini na baadhi ya wageni waalikwa wakiwa kwenye hafla ya kupokea ndege moja iliyonunuliwa kwa lengo la kudhibiti visumbufu mimea leo Mei 30, 2025 kwenye Kiwanja kidogo cha Ndege Jijini Dodoma. Waziri wa...

TIMU YA UMITASHUMTA 2025 MKOA WA DODOMA YASISITIZWA NIDHAMU,UPENDO NA KUJITUMA

Image
  Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mkoa wa Dodoma ambaye ni Afisa Elimu Taaluma Mwalimu Justin Machela, akihamasisha timu ya UMITASHUMTA Mkoa kuwa na nidhamu, upendo na kujituma  wakati wa hafla fupi ya kutangaza timu ya Mkoa itakayowakilisha kwenye mashindano hayo Kitaifa Mkoani Iringa iliyofanyika katika  Shule ya Sekondari Dodoma leo Mei 30, 2025. Afisa Michezo Mkoa wa Dodoma Bw. Evance Sangawe akitangaza majina ya wanamichezo watakao wakilisha Mkoa kwenye michezo ya UMITASHUMTA 2025 Kitaifa Mkoani Iringa wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika  Shule ya Sekondari Dodoma leo Mei 30, 2025. Mwenyekiti wa Umoja wa Walimu Wakuu Tanzania (TAPSHA) Mwalimu James E. Manary akizungumzia msaada walioutoa kuunga mkono juhudi za Mkoa katika kuhudumia kambi ya timu ya UMITASHUMTA 2025  wakati wa hafla fupi ya kutangaza timu hiyo itakayowakilisha Mkoa kwenye mashindano hayo Kitaifa Mkoani Iringa iliyofanyika katika  Shule ya Sekonda...

WANAFUNZI WAHIMIZWA KUENDELEZA VIPAJI WALIVYONAVYO KWAKUWA NI FURSA YA AJIRA.

Image
  Na; Happiness E. Chindiye        Habari - Dodoma RS Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule amewataka wanafunzi wa Shule za Msingi kutoka Halmashauri zote nane za Mkoani hapa ambao wapo katika kambi ya siku saba ya kuandaa timu itakayowakilisha Mkoa kwenye mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) yatakayofanyika Kitaifa Mkoani Iringa kuendeleza vipaji walivyonavyo kwa kuwa ni fursa ya ajira kwa siku zijazo. Wito huo umetolewa  Mei 27,2025 wakati akizindua rasmi mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa ambayo yanalenga kuunda timu ya Mkoa itakayowakilisha kwenye mashindano ya Kitaifa yatakayofanyika mkoani Iringa kuanzia Juni 08 mwaka huu.   “ Mkoa wa Dodoma tunasema ni fahari ya Watanzania, tunataka isiwe kwenye elimu peke yake tunataka iwe kwenye mchezo na sekta nyingine zote.Hakikisheni kwa hii wiki moja mnajifunza vizuri ili mkatuwakilishe Kitaifa na mshike namba moja hivyo tumieni hii wiki vizu...

UHAKIKI ANUANI ZA MAKAZI KUANZA MEI 28 DODOMA

Image
  Na Sizah Kangalawe Habari- DodomaRS Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar Mmuya amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanasimamia kwa ukamilifu zoezi la uhakiki wa taarifa za  anuani za makazi, linalotarajia kuanza Mei 28/ 2025 katika Halmashauri za Mkoa wa Dodoma. Mmuya amesema hayo wakati wa uzinduzi wa zoezi la Uhakiki wa Taarifa hizo Mei 26/2025, Katika ukumbi wa Mikutano wa Four point Hotel Jijini Dodoma, uliowahusisha watendaji kata, wenyeviti wa Serikali za mitaa na vijiji na Maafisa  Tarafa. ‘’Wakurugenzi wote, hakikisheni mnasimamia zoezi hili katika halmashauri zenu huku mkitambua kuwa ni zoezi endelevu hivyo sitegemei kusikia mmeacha kuhuisha taarifa baada ya siku za zoezi hili kumalizika. ‘’Vilevile hakikisheni mnatumia Mfumo wa anuani za makazi kutambua  makazi na wakazi katika maeneo yenu ili kuongeza ufanisi katika kusimamia mazoezi mbalimbali ya kitaifa na kupanga mipango ya maendeleo’’, Amesema Mmuya Akitoa salamu za Jiji la Dodoma Mey...

KAMPENI YA ‘GURUDUMU LA MAMA SAMIA’ - MATOKEO YA IMANI YA SERIKALI KWA SEKTA BINAFSI

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akizungumza na Maafisa Usafirishaji wa Bodaboda na Bajaji wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya 'Gurudumu la Mama Samia' iliyoanzishwa na Kampuni ya 'Road Master' na kufanyika kwenye viwanja vya soko la Machinga Jijini Dodoma Mei 28, 2025. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri akizungumza na Maafisa Usafirishaji wa Bodaboda na Bajaji wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya 'Gurudumu la Mama Samia' iliyoanzishwa na Kampuni ya 'Road Master' na kufanyika kwenye viwanja vya soko la Machinga Jijini Dodoma Mei 28, 2025. Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Anthony Mavunde akizungumza na Maafisa Usafirishaji wa Bodaboda na Bajaji wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya 'Gurudumu la Mama Samia' iliyoanzishwa na Kampuni ya 'Road Master' na kufanyika kwenye viwanja vya soko la Machinga Jijini Dodoma Mei 28, 2025. Mkurugenzi wa Kampuni ya 'Road Master Bw. Fuein Makamba akizungumza na Maafisa Usafirishaji wa ...

WAWEKEZAJI WA VIWANDA KUTOKA DUBAI WABISHA HODI DODOMA

Image
  Na. Hellen M. Minja        Habari – DODOMA RS Ikiwa ni siku moja tu baada ya ziara ya Kidiplomasia (Capital City Diplomatic Tour) iliyowahusisha mabalozi kutoka nchi mbalimbali Duniani Jijini Dodoma,Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amepokea ugeni kutoka nchini Dubai kuzungumzia juu ya upatikanaji wa fursa za uwekezaji wa ardhi  kwa ajili ya kujenga viwanda kwa kuzingatia Dodoma inazidi kukua kutokana na hadhi yake ya Makao Makuu ya nchi na kupokea wageni wengi wa ndani na nje ya nchi. Wawekezaji hao ambao ni Bw. Emmanuel Salinos na Bw. Walid Jumaa, wamefika ofisini kwa Mkuu wa Mkoa Jengo la Mkapa Jijini Dodoma Mei 28, 2025 ambapo hii ni mara ya pili kufika hapa kwa ajili ya dhumuni hilo ingawa awali waliona Dodoma haijakua kama ilivyo sasa. Aidha, lengo hasa la wawekezaji hao ni kutafuta eneo lenye ukubwa wa ekari 1,000 kwa ajili ya kuwekeza na kutengeneza Mji unaofanana na Dubai ambapo wataleta wawekezaji wengine kutoka nchini mwao kwani ...

VIONGOZI KUTOKA TUME YA MADINI WAMTEMBELEA RAS MMUYA

Image
  Uongozi kutoka Tume ya Madini ukiongozwa na Mwenyekiti wake Bi. Janeth Reuben Lekashingo wamemtembelea Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya ofisini kwake leo tarehe 28.05.2025. Ugeni huo umefika ofisini hapo kwa lengo la kujitambulisha na kutoa taarifa ujio wa ziara yao ndani Mkoa huu.  Bw. Mmuya akipokea salamu hizo ametumia wasaa huo kuwa taarifu vipaumbele vya Mkoa huu ndani ya mwaka 2025 vikiwa ni pamoja na utalii, madini na Kilimo. #dodomafahariyawatanzania #wekezadodomastawishadodoma #keroyakowajibuwangu #mtiwangubirthdayyangu