Posts

Showing posts from January, 2023

UKILETWA DODOMA UMELETWA KUJENGA MAKAO MAKUU YA NCHI

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amemuapisha Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe. Gerald R. Mongella pamoja na kuwapokea Wakuu wa Wilaya wapya wawili waliohamishiwa Mkoa wa Dodoma kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa jengo la Mkapa zilipo Ofisi za Mkuu wa Mkoa. Mhe. Senyamule amewaasa Wakuu hao wa Wilaya kuheshimu nafasi waliyopewa na Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwani wameaminika kuitumikia nafasi hiyo. “Nafasi ya Ukuu wa Wilaya ina madaraka na dhamana kubwa sana, ukiyatumia kwa tija yanaleta manufaa ila ukiyatumia vibaya utakwenda kupata matokeo mabaya” Aidha Mhe. Senyamule amesema kuwa Dodoma ni Makao Makuu ya nchi na nafasi waliyopewa wakuu hao  ni kuja kuijenga Makao Makuu. “Kuja Dodoma ni bahati kwakuwa mnakuwa sehemu ya kujenga Makao Makuu ya nchi. Yeyote aliyekuja hapa, ajue amepata nafasi ya kujenga Makao Makuu kwani viongozi wetu wakuu wana matarajio makubwa na sisi. Mkoa umejipanga kuifanya Makao Makuu kama yalivyo matarajio ya viongozi wetu” Mhe....

KATIBU TAWALA MKOA WA DODOMA DKT. FATUMA MGANGA AFUNGUA MAFUNZO YA PROGRAM YA SHULE BORA KWA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA DODOMA

Image
Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Dkt Fatuma Mganga ametoa rai kwa waandishi wa habari wanaofanya kazi ndani ya Mkoa huo kutangaza mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya elimu  pamoja na kuyatangaza kwa jamii. Rai hiyo ameitoa Januari 27, 2023 Wilayani Kondoa wakati akifungua mafunzo ya Siku Moja kwa maafisa habari na waandishi wa habari, yenye lengo la kuwajengea uwezo kufahamu Mradi wa Shule Bora na kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu Katika masuala ya elimu.  Akizungumzia suala la maendeleo ya Elimu Katika Mkoa amesema suala la Elimu katika Mkoa wa Dodoma bado halijatangazwa vizuri na kuwataka waandishi wa habari wakawe chachu cha kuielimisha jamii. Pia amempongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za dhati za kuongeza pesa za maendeleo katika mkoa wa Dodoma ambapo shilingi bilioni 7.8 zimetolewa na kuwezesha kujenga vyumba vya madarasa 393 kwa Shule za Msingi na madarasa 130 yamejengwa kwa Shule za Sekondari yamejengwa kwa gharama ya shilingi Bil...

WANAWAKE SIMAMENI KWENYE NAFASI ZENU ZA MALEZI

Image
Wito umetolewa kwa wanawake kusimama kwenye nafasi zao za malezi kwa watoto ili kutengeneza jamii yenye maadili. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule alipokuwa akitoa hotuba yake wakati wa Kongamano la wasichana wa Baraza la Kiislamu Tanzania BAKWATA lililofanyika kwenye eneo la Msikiti wa Gaddafi Jijini Dodoma. Kongamano hilo lililoandaliwa na BAKWATA kwa wasichana, limelenga kujadili mambo mbalimbali yanayowakabili wasichana kwenye jamii hasa kukithiri kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na vitendo vya ukatili kwa watoto na wanawake katika jamii zetu. "Wanawake tusimame kwenye nafasi zetu za malezi ya watoto kwani maadili yameharibika nyakati hizi ndio mana kuna wimbi kubwa la vitendo vya unyanyasaji na ukatili kwa watoto na wanawake. Tukishirikiana na kuamua kwa pamoja kutokomeza vitendo hivi, hakuna linaloshindikana" Amesema Mhe Senyamule Aidha amefafanua suala la mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa kundi la wanawake na kuwaondolea hofu ya...

MHE.SENYAMULE ATEMBELEA MAONESHO YA WIKI YA SHERIA

Image
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyumule ametembelea maonesho ya wiki ya sheria yalioanza tarehe 22/1 hadi 29/1 wadau walioshiriki kutoa Elimu kwenye maonesho hayo ni 35. Akizungumza na wadau hao Senyamule amesema niwapongeze kuimili wa mahakama  kwa kazi nzuri wanazoendelea kuzifanya ambazo kwa wiki ya sheria  tumepata nafasi na wanachi kushuhudia   mabadiliko makubwa na mapinduzi mabukwa ambazo kwenye muimili wa sheria tunaon vitabu na vipeperushi vikitafsiliwa kwa lugha ya  Kiswahili. “tumepata nafasi ya kushuhudia mabanda mengi yakitoa elimu juu ya muimili wa mahaka na watu weng wanpnda suruhishi kama njia ya kwanza ya kutoa matatizo kabla ya kutoa ukumu  na kama kauli mbiu inavosema ya Mahakam sasa tunaneda kutoa suruhishi. Elimu zitolewe kwa kila mwanachi ili kwakila mtu ajue juu ya sheria ya Mahakam  na hitaongeza juhudi  juu ya kutoa haki na mapatano juu ya kila tatizo mabalo  mwananchi hanapaswa kujua haki ...

MHE. SENYAMULE AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI LATRA

Image
                                         Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amezindua rasmi Baraza la wafanyakazi  wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri ardhini  LATRA katika kikao  cha kwanza cha Baraza la wafanyakazi kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa LATRA makao makuu Dodoma. Akizungumza na wafanyakazi Senyamule amesema anawapongeza kwa kukamilisha taratibu za kisheria za kuunda baraza hili na Kusajiliwa na Kamishna wa kazi viongozi wa chama cha cummunication and workers traders union (COWTU) Taifa na Tawi la LATRA  kwa kuwezesha kufikia makubaliano na Menejimenti ya LATRA kwa kusaini mkataba na kuunda baraza la kwanza la wafanyakazi wa Mamlaka hii ‘’Katika kuendeleza mshikamano hapana budi Menejimenti ihakikishe kwamba haki za msingi za mtumishi zinatolewa  juhudi zitolewe katika kujifunza kujiendekeza kimasomo ili kuendeleza ufanisi wa kazi na kujiwekea misingi imara ya ...

IBADA YA MAZISHI YA ALIYEKUWA KATIBU TAWALA MSAIDIZI RASILIMALI WATU MKOA WA DODOMA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameshiriki kwenye mazishi ya aliyekuwa Katibu Tawala Msaidizi (Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu) Bw. Aloyce Mwogofi katika ibaada ya mazishi iliyofanyika Mkoani wa Njombe, Kijiji cha Itulike Kata ya Ramadhani. Akizungumza na wafiwa na waombolezaji Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amewataka waombolezaji kuiga mwenendo wake kwa kuiga mambo mema yoye aliyotekeza enzi za uhai wake. “Mzee Mwogofi alikuwa ni mchapa kazi kwa asili yake, muadilifu na mfano wa kuigwa kuanzia vitendo, mavazi, nidhami na kwa kuwa kiongozi wa wa utumishi aliongoza wengine kwa mfano”Alisisitiza Bi. Senyamule. Kama Serikali tunasema mapengo haya zibiki kwa maana hatutampata Mzee Mwogofi mwingine lakini tunaomba Mwenyezi Mungu atusaidie tupate mtu ambaye hatutaona hasara kubwa ya kumpoteza Mzee Mwogofi kwa maana ya alivokuwa. "Mungu awashike Mkono familia awatie nguvu endeleeni kumtegemea Mungu leo tunamlaza Mzee wetu tuendelee kuiga mfano wa mzee wetu na tuige ...

MKOA WA DODOMA WAAINISHA MAKUBWA YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA, YATANGAZA MAFANIKIO YAKE

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Philip Isdor Mpango amehimiza wananchi wa Dodoma kufanya kazi kwa bidii ili kuinua uchumi wa Mkoa na nchi nzima kwa ujumla. Dkt. Mpango ameyasema hayo leo katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na   Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Angela Kairuki katika ukumbi wa Kanisa la TAG - Mipango katika Mkutano wa kutangaza Mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Serikali kwa kipindi cha Miaka Miwili (2021/2022- 2022/2023 )   "Licha ya anguko la kiuchumi Duniani kufuatia ugonjwa wa UVIKO - 19 pamoja na vita inavyoendelea huko Ukraine, bado uchumi wetu umeendelea kukua na tunatarajia kufikia hadi 5.0% na Dodoma inakua na kuchangia 3.1%ya pato la Taifa. Nawahimiza wananchi wa Dodoma kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha mchango wao katika pato la Taifa unaendelea kukua" Amesisitiza Mhe. Mpango. Kadhalika, ameongelea pia suala la elimu kwa kusisitiza wazazi na walez...

MRADI WA REST WAZINDULIWA DODOMA

Image
           Mkoa wa Dodoma umezindua rasmi mradi unaoshughulikia masuala ya afya ya uzazi kwa vijana, wanawake na watoto unaojulikana kama Reproductive Equity Strategic (REST) unaoendeshwa na shirika lisilo la Kiserikali la Deutsche Shiftung Weltbevolkerung (DSW) - Tanzania ambao utafanya kazi kwenye Wilaya tatu za Mkoa ikiwa ni pamoja na Dodoma mjini, Bahi na Mpwapwa. Mradi huo umezinduliwa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Rosemary Senyamule kwenye kikao kilichofanyika ukumbi wa jengo la Mkapa. Akizindua mradi huo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema Serikali ya Awamu ya Sita imetoa kipaumbele katika sekta ya afya ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu yake ili kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora ya afya. “Matokeo ya sensa ya mwaka 2022 yanaonyesha kuwa Tanzania ina jumla ya hospitali 676, vituo vya afya 1,466 na zahanati 7, 965. Tanzania Bara pekee ina hospitali 662, vituo vya afya 1,430 na zahanati 7,680 na mkoa wetu wa Dod...