Posts

Showing posts from February, 2025

RC SENYAMULE NA MIKAKATI YA KUKUZA UCHUMI WA WANANCHI DODOMA

Image
  Na. Hellen M. Minja,         Habari – DODOMA RS Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amekutana na Menejimenti ya Ofisi yake Februari 26, 2025, katika kikao kazi cha kujadili utendaji kazi pamoja na kupanga mikakati ya kuwezesha Mkoa kufikia malengo yake kwa mwaka huu 2025 katika ukumbi wa Hoteli ya Residence, Mipango Jijini Dodoma.  Kikao hicho kiliambatana na ajenda kadhaa ikiwemo uwasilishaji wa taarifa za utekelezaji wa bajeti kuanzia mwezi Juni – Desemba, 2024, mkakati wa ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa Mkoa wa Dodoma. Aidha, Mhe. Senyamule ameitaka menejimenti hiyo kuwa na mikakati ya kukuza uchumi wa Mkoa kwani kipaumbele cha Mkoa mwaka huu ni kupandisha uchumi wa wananchi wake ili waweze kuondokana na umasikini.   #dodomafahariyawatanzania #keroyakowajibuwangu #mtiwangubirthdayyangu

RS DODOMA NA UTAMADUNI WA CHAKULA CHA PAMOJA: MWEZI FEBRUARI .

Image
  Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Thomas Rutachunzibwa aliyemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule kwenye hafla fupi ya chakula cha mchana pamoja na watumishi wa ofisi hiyo sambamba na kusheherekea kumbukizi za siku za kuzaliwa kwa watumishi waliozaliwa mwezi Februari katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa jengo la Mkapa Jijini Dodoma Keki na Shampeni maalumu zilizoandaliwa kwa ajili ya kusheherekea kumbukizi ya siku za kuzaliwa kwa watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma waliozaliwa mwezi Februari iliyofanyika jana Februari 26, 2025 kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa jengo la Mkapa Jijini Dodoma Baadhi ya wazaliwa wa mwezi Februari wakishirikiana kukata keki kwa niaba ya wenzao wakati wa hafla ya chakula cha pamoja kwa watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ambayo kama ilivyo ada huambatana na sherehe hizo kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa jengo la Mkapa Jijini Dodoma. Baadhi ya wazaliwa wa mwezi Februari wakishirikiana kumlisha keki mgeni ras...

VIFAA VYOTE VYA UJENZI VINUNULIWE NA VIWEPO ENEO LA UJENZI-RAS MMUYA.

Image
  Na.Sofia Remmi  Habari- RS Dodoma  Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw.Kaspar  K. Mmuya amefanya ziara ya kukagua miradi ya Kimkakati Katika Halmashauri ya Wilaya za Chemba na Kondoa Mji, Februari 25,2025 . Katika ziara hiyo Katibu Tawala  alitembelea; Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari Maalum ya wavulana ya Kanda inayogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 4,1000,000,000.Mradi wa Shule Mpya ya Sekondari Kidoka  unaogharimu kiasi cha Shilingi 443,597,084 na mradi wa Shule Mpya ya Sekondari ya Ufundi wa Amali Kata ya Kingale inayogharimu kiasi cha shilingi 544,225,626.00 Akizungumza akiwa katika ziara hiyo, Katibu Tawala Mmuya amesema,  "Mhe.Rais ametoa fedha nyingi kwenye miradi hii ya kimkakati, jukumu  lililobaki lipo kwenu la kununua vifaa vyote na viwepo eneo la ujenzi na sio mtu anajiamulia tu kununua vifaa kidogo kidogo,jambo hilo hapana vifaa vinunuliwe vyote. Mradi hii itakuja kuwasaidia sana Vijana wetu, hivyo muda uliopangwa kukamilisha...

RAS MMUYA ATOA SALAMU ZA POLE KWA FAMILIA YA MAREHEMU MAGUO.

Image
  Na Sofia Remmi. Habari-Dodoma Rs Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw.Kaspar K.Mmuya ametoa salamu za Pole kwa Familia na waombolezaji mbalimbali kufuatia kifo cha Mhe. Abdallah Maguo aliyekuwa Diwani na Mwenyekiti na Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, aliyefariki tarehe 24 Februari 2025,katika hospitali ya Benjamin Mkapa wakati akipatiwa matibabu. RAS Mmuya amewaombea faraja ya mwenyezi Mungu iwafikie familia,ndugu,jamaa na marafiki walioguswa na msiba huo. Akizungumza na waombolezaji RAS  Mmuya amesema marehemu Maguo alikuwa muadilifu aliyezingatia maadili ya kazi yake ya kuwatumikia wananchi wake wa Kata ya  Mnenia wakati wote. “ Jambo la msiba si jambo la kuzoeleka, na njia pekee ya Kumuenzi Maguo ni kuyaenzi mema yake ya wakati wote kipindi cha uhai wake. Muda wa kuishi duniani ni mfupi sana tunapaswa kutenda mema wakati wote sio kwa ajili yetu,bali kwa ajili ya wote” Amesema Mmuya.  Aidha msiba huo umefanyika Katika Kijiji cha Mnenia kata ya Mnenia Halmashauri ya Wi...

MAKALA FUPI KUELEKEA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Image
  Na: Hellen M. Minja, Habari - DODOMA RS  Maadhimisho ya kilele cha siku ya Wanawake Duniani, hufanyika kila mwaka ifikapo Machi 08. Kuelekea maadhimisho hayo Kitaifa 2025, yanayotarajiwa kufanyika Mkoani Arusha, huku Mgeni rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Mikoa ya Dodoma,Singida na Iringa  imeandaa Kongamano kubwa litakalowakutanisha Wanawake wa mikoa hiyo, Mkoa wa Dodoma ukiwa mwenyeji wa Kongamano hilo  litakalofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma Machi 03, 2025. Lengo la Kongamano hilo ni  kumtambua Mwanamke katika nafasi ya Uongozi,ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Spika Mstaafu wa Bunge la  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Anna Makinda. Ni  hatua muhimu katika mfumo wa maisha ya mwanadamu inayolenga kuhakikisha kuwa na fursa sawa kwa wote na kushiriki kwenye Uongozi na maamuzi yote katika jamii. Kongamano hilo pia litasadifu lengo la maadhimisho ya siku ya Mwanam...

KUOKOA MAISHA YA MAMA NA MTOTO MAANA YAKE TULENGE VIFO SIFURI : RAS MMUYA

Image
Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar Mmuya Februari 24/ 2025, ametembelea Hospitali ya rufaa  ya Mkoa wa Dodoma kwa lengo la kufanya ufuatiliaji akilenga huduma ya Mama na Mtoto.  Katika ziara hiyo Bw. Mmuya aliambatana na Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Thomas Rutachunzibwa pamoja na watendaji wengine kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa . Akizungumza akiwa hospitalini hapo Mmuya amesema "Sisi tuna jukumu la kulinda Afya ya Mama na Mtoto,maelekezo ya Mheshimiwa Rais kwa watendaji wake ni nendeni mkasimamie eneo hili.Yeye Mhe. Rais amewekeza vya kutosha kuzuia vifo vya Mama na Mtoto,sisi hatumdai, lakini yeye anatudai sisi.Mmeapa kuokoa maisha ya watu,hakikisheni mnafanya hivyo. Kuokoa maisha ya Mama na Mtoto,maana yake tulenge 'zero death'.Tuendelee kufanya kazi kwa bidii,kwa kujiamini,lengo letu likiwa ni kuona watu wanaendelea kubaki na uhai wao.Kila mtu afanye kazi yake,hata ifike mahali moyo wako useme,nilifanya 'to the best' ". Aidha Daktari  Rutachunzibwa,amemshuku...

DKT. MSONDE AMTEMBELEA RAS DODOMA KWA MAZUNGUMZO

Image
  Na. Hellen M. Minja,         Habari – DODOMA RS Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Dkt. Charles Msonde, leo Februari 24, 2025, amemtembelea Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya Ofisini kwake Jengo la Mkapa Jijini Dodoma kwa lengo la kuzungumza juu ya mabadiliko ya mfumo wa malipo kwa huduma kutoka kwa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania, TEMESA. Dkt. Msonde amemueleza Katibu Tawala Mkoa kwamba, Wakala huyo anapitia changamoto mbalimbali zinazosababisha kulemewa na mzigo wa madeni kutokana na huduma wanazozitoa kushindwa kulipiwa kwa wakati hasa utengenezaji wa magari ya Serikali. “Tumekuja na mapendekezo kwa Serikali ambayo yamepitishwa na Mhe. Rais kwamba kuanzia Januari, 2025, Mfumo wa malipo ya huduma kwa TEMESA yatakua kwa ‘pre-paid’, kama utapeleka gari pale basi ulipie kabla au baada ya matengenezo kwa control namba na lengo ni kufikia Julai mosi 2025, mwaka mpya wa fedha, hatutaki kusikia TEMESA inadaiwa” Dkt. Msonde. Aidha, Bw. Mmuya am...

PBZ WAMTEMBELEA KATIBU TAWALA MKOA WA DODOMA

Image
  Na.Sofia Remmi. Habari-Dodoma Rs Uongozi wa Bank ya PBZ umemtembelea Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma  Bw. Kaspar K. Mmuya ofisini kwake jengo la Mkapa Jijini Dodoma,mapema Februari 19,2025. Lengo la ziara hiyo ni kusalimia na  kuzungumza kuhusu fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo katika Mkoa wa Dodoma. Uongozi huo uliambatana na Meneja wa Benki ya PBZ Dodoma Bi. Mwanaharusi Ally na Afisa Mahusiano Abdul Khamis. #dodomafahariyawatanzania. #keroyakowajibuwangu.

MTI WANGU, BIRTHDAY YANGU FEBRUARI YAFANYIKA NZUGUNI

Image
  Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar Mmuya, akizungumza umuhimu wa kupanda miti wakati wa hafla ya kampeni ya Mti wangu Birthday yangu kwa mwezi Februari iliyofanyika kwenye viwanja wa Nanenanae, Nzuguni Jijini Dodoma Februari 18, 2025 Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Utunzaji Mazingira na Ufugaji wenye Tija Bw. Jeremia John Wambura ambaye ni moja ya mdau aliyealikwa kwenye hafla ya kampeni ya Mti wangu Birthday yangu kwa mwezi Februari akizungumza kwenye viwanja wa Nanenanae, Nzuguni Jijini Dodoma Februari 18, 2025  Afisa TEHAMA kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ambaye pia ni mzaliwa wa Februari Bi Grace Moshi akizungumza kwa niaba ya wazaliwa wote wakati wa hafla ya kampeni ya Mti wangu Birthday yangu kwa mwezi Februari iliyofanyika kwenye viwanja wa Nanenanae, Nzuguni Jijini Dodoma Februari 18, 2025 Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar Mmuya, akipanda mti wakati wa hafla ya kampeni ya Mti wangu Birthday yangu kwa mwezi Februari iliyofanyika kwenye viwanja wa Na...