Posts

Showing posts from January, 2025

WATUMISHI WA OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA MAZOEZINI

Image
Na. Sizah Kangalawe Habari- Dodoma Rs.  Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  Dodoma, Leo Ijumaa Januari 31, 2025 wamefanya mazoezi ya viungo vya mwili Ili kuimarisha Afya zao.  Mazoezi hayo yalifanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Amani Jijini Dodoma, ikiwa ni muendelezo wa utaratibu waliojiwekea wa kufanya mazoezi kila siku ya Ijumaa ya Juma baada ya kumalizika saa za kazi na Kila jumamosi ya mwisho wa mwezi.  Dhamira ya Mazoezi hayo ni kuimarisha Afya, kuepuka magonjwa yasiyoambukiza pamoja na kuimarisha mahusiano na Mshikamano baina yao.  

MKOA WA DODOMA WAENDELEA NA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA KIFUA KIKUU

Image
  Mratibu wa Huduma za kudhibiti Kifua Kikuu kutoka Wizara ya Afya Dkt. Allan Tarimo, akizungumzia malengo matatu ya Mpango wa kuibua wagonjwa wenye vimelea vya Kifua Kikuu wakati wa Kikao kazi cha vituo vya huduma za Afya binafsi vinavyotoa huduma za ugonjwa huo pamoja na wadau kilichofanyika kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jengo la Mkapa Jijini humu leo Januari 31, 2025 Mratibu wa Kifua Kikuu na ukoma Mkoa wa Dodoma Dkt. Peres Lukango (aliyesimama) akielezea hali ya utoaji huduma za Kifua Kikuu  wakati wa Kikao kazi cha vituo vya huduma za Afya binafsi vinavyotoa huduma za ugonjwa huo pamoja na wadau kilichofanyika kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jengo la Mkapa Jijini humu leo Januari 31, 2025 Picha juu na chini, baadhi ya watoa huduma kutoka vituo binafsi vya huduma za afya hususan Kifua Kikuu na wadau mbalimbali wakifuatilia Kikao kazi kilicholenga kufanya tathmini ya uibuaji wa wagonjwa wenye vimelea vya ugonjwa huo kilichofanyika kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mko...

HUDUMA ZA KISHERIA ZATOLEWA DODOMA KUELEKEA FEBRUARI PILI

Image
  Mtoa huduma za Kisheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi Rose Mtani akimuelekeza mwananchi kuweka sahihi kwenye kitabu cha wageni pindi alipotembelea Banda la Sheria la Mkoa linalopatikana kwenye viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma likitoa huduma kuelekea maadhimisho ya kilele cha wiki ya Sheria Februari 02, 2025. Mtoa huduma za Kisheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi Rose Mtani, akimsikiliza mwananchi aliyetembelea Banda la Sheria la Mkoa linalopatikana kwenye viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma juu ya changamoto yake inayohitaji msaada wa kisheria kuelekea maadhimisho ya kilele cha wiki ya Sheria Februari 02, 2025. Na. Sizah Kangalawe Habari- Dodoma Rs  Ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Sheria Nchini yanayofanyika katika viwanja vya 'Nyerere Square' Jijini Dodoma, Banda la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Kupitia kitengo Cha Sheria linapatikana katika viwanja hivyo. Huduma mbalimbali za kisheria zinatolewa katika banda hilo pasi na gharama yoyote...

WAZIRI MKUU WA UGANDA AZURU KIWANDA CHA ITRACOM DODOMA.

Image
Picha juu na chini, Waziri Mkuu wa Uganda Mhe. Robinah Nabbanja (wa pili kulia) akisalimiana na wenyeji wake alipowasili kwenye kituo cha Treni ya kisasa ya SGR Mkonze Jijini Dodoma, pindi alipofika Mkoani hapa kwa ajili ya kufanya ziara ya siku moja kwenye kiwanda cha mbolea cha Itracom kilichopo Kata ya Nala Jijini Dodoma jana Januari 29, 2025. Waziri Mkuu wa Uganda Mhe. Robinah Nabbanja (katikati) akiwa na wenyeji wake Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Selemani Jafo (kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule (wa kwanza kulia) pamoja na viongozi wa kiwanda cha mbolea Itracom Jijini Dodoma, wakati  alipotembelea kiwanda hicho Januari 29, 2025 kujionea namna uzalishaji wa mbolea ya kisasa unavyofanyika. Waziri Mkuu wa Uganda Mhe. Robinah Nabbanja (katikati) akiwa na wenyeji wake Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Selemani Jafo (wa kwanza kulia, mbele), Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule (wa pili kulia) kwenye moja ya chumba cha kuhifadhia mbolea iliyokwi...

RC SENYAMULE AZINDUA BODI YA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akizungumza na Wajumbe wa Bodi mpya ya Hospitali ya Rufaa ya  Mkoa wa Dodoma sambamba na wadau wengine wakiwemo Watumishi wa Hospitali hiyo wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Bodi hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Hospitali Jijini Dodoma leo Januari 29, 2025. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akizindua rasmi Bodi ya Hospitali ya Rufaa ya  Mkoa wa Dodoma wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Hospitali hiyo Jijini Dodoma leo Januari 29, 2025. Baadhi ya Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya  Mkoa wa Dodoma wakifuatilia zoezi la uzinduzi wa Bodi ya Ushauri ya Hospitali hiyo wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Hospitali Jijini Dodoma leo Januari 29, 2025. Picha juu na chini, baadhi ya Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Rosemary Senyamule alipokua akizungumza na Wajumbe wa Bodi mpya ya Hospitali hiyo wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa...

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akitoa maagizo kwa walimu (hawapo pichani) kuhusu kufundisha uzalendo kwa wanafunzi wa shule ya msingi Kusila Wilaya ya Bahi wakati alipofanya ziara ya kikazi kukagua miradi ya miundombinu inayoendelea kutekelezwa katika shule hiyo mnamo Januari 28, 2025.  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule (katikati) akisalimiana na wanafunzi wa shule ya msingi Kusila Wilaya ya Bahi wakati alipofanya ziara ya kikazi kukagua miradi ya miundombinu inayoendelea kutekelezwa katika shule hiyo mnamo Januari 28, 2025.  Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Dodoma pamojna na Wataalamu mbalimbali waliombatana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule (hayupo pichani) wakifuatilia maagizo yaliyotolewa juu ya kufundishwa uzalendo wanafunzi wa shule ya Msingi Kusila Wilaya ya Bahi. Picha juu na chini, baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Mwitikira katika Wilaya ya Bahi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh...

DODOMA NA SHAMRASHAMRA ZA KUMBUKIZI YA SIKU YA KUZALIWA YA MHE RAIS .

Image
  Ikiwa ni muendelezo wa matukio ya kuenzi  kumbukizi ya siku ya  kuzaliwa ya Dkt. Samia Suluhu Hassan,viongozi mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi na Serikali wakiongozwa na Ndg. John Mongella,wamejumuika kumpongeza na kusheherekea. Hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Mikutano makao makuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) leo tarehe 27 Januari 2025.

KLABU YA MAZINGIRA PALACE SCHOOL YAMTEMBELEA RC SENYAMULE

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akizungumza na wanafunzi wa Klabu ya Mazingira kutoka shule ya msingi Palace ya Jijini Dar Es Salaam (hawapo pichani) walipofika ofisini kwake Jengo la Mkapa Jijini Dodoma leo Januari 27, 2025 kwa lengo la kumpongeza kwa jitihada zake za kutunza mazingira kwa kupanda miti, hususan kwenye kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Rais wa Tanzania. Mkuu wa shule ya Palace ya Jijini Dar Es Salaam Mwalimu Ferdinand E. Ilungu, akielezea lengo la ujio wa Klabu ya Mazingira ya shule yake kwenye Mkoa wa Dodoma ambalo ni kuunga mkono jitihada za kulinda mazingira kwa kupanda miti pindi walipomtembelea Mkuu wa Mkoa huu Ofisini kwake jengo la Mkapa Jijini Dodoma leo Januari 27, 2025 Klabu ya Mazingira kutoka shule ya msingi Palace ya Jijini Dodoma walipofika ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule Jengo la Mkapa Jijini Dodoma ili kumpongeza kwa jitihada za kutunza mazingira kupitia kampeni mbalimbali za kupanda miti hususan siku ya le...

RC SENYAMULE ATOA MSAADA WA MABATI KWA WAHITAJI

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akimkabidhi fedha taslimu shilingi milioni moja Bw. Kombo Jumbe ofisi kwake Jengo la Mkapa Jijini Dodoma ikiwa ni msaada wa kununua mahitaji ya kumalizia kuezeka nyumba yake aliyojenga mpaka kiwango cha lenta. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule (katikati) akiwakabidhi msaada wa mabati ya kuezekea nyumba zao Bw. Kombo Jumbe (kulia) na Bi. Farida Saidi ambao wote wamejenga kufikia kiwango cha lenta lakini wakashindwa kuezeka kutokana na changamoto mbalimbali. Na. Hellen M. Minja,         Habari – DODOMA RS Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, leo Januari 27, 2025, ametoa msaada wa mabati na fedha taslimu shilingi Milioni Moja kwa wakazi wawili wa Mkoa wake wenye mahitaji maalum ambao wote wamefanikiwa kujenga nyumba hadi hatua ya lenta lakini wameshindwa kupaua kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili. Akikabidhi msaada huo, kwenye viwanja vya ofisi yake Jengo la Mkapa Jijini Dodoma, M...

DODOMA WAPANDA MITI 1,480 KUADHIMISHA BIRTHDAY YA MHE. RAIS

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akizungumzia umuhimu wa kupanda miti baada ya kukamilika kwa zoezi hilo lililoashiria hafla ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyofanyika kwenye eneo la viwanja vya Nanenane, Nzuguzi Jijini Dodoma leo Januari 27, 2025   Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, akiotesha mti kama ishara ya kuunga mkono kampeni ya birthday yangu mti wangu wakati wa hafla ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyofanyika kwenye eneo la viwanja vya Nanenane, Nzuguzi Jijini Dodoma leo Januari 27, 2025 Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya akiotesha mti kama ishara ya kuunga mkono kampeni ya birthday yangu mti wangu wakati wa hafla ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyofanyika kwenye eneo la viwanja vya Nanenane, Nzuguzi Jijini Dodoma leo Januari 27, 2025 Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Dodoma Mhe. Fatma To...