Posts

Showing posts from October, 2024

RC SENYAMULE ATATUA MGOGORO WA UJENZI WA SHULE KIDOKA - CHEMBA

Image
Na. Hellen M. Minja,                 Habari – DODOMA RS Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule, leo Oktoba 31, 2024, ametatua mgogoro kati ya wananchi wa Kata ya Kidoka juu ya ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kata, kufuatia Wananchi wa  vijiji viwili vya Kidoka na Pangalua  vilivyoko katika kata ya Kidoka,Halmashauri ya wilaya ya Chemba, wote kutaka   shule ijengwe kwenye vijiji vyao. Mkuu wa Mkoa huyo ametatua mgogoro huo wakati wa mkutano wa hadhara kwenye Kijiji cha Pangalua,mkutano ambao lengo lake ni  kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili wakazi wa kata hiyo,ikiwemo eneo la ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kata. “Serikali imeona wote mna mahitaji ya shule, mabishano haya yanatokana na dhamira njema, japo inatuchelewesha kwani ilitakiwa kufanyiwa maamuzi ya haraka. Tumeamua shule zijengwe mbili, kwa maana ya Kidoka na Pangalua. Shule mbili zitajengwa, kila Kijiji  kipate ya kwake” Amesema Mhe. Se...

WATUMISHI WA OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA WASHIRIKI HAFLA YA CHAKULA CHA MCHANA

Image
Na Sofia Remmi  Habari-Dodoma Rs Katibu tawala mkoa wa Dodoma Bw.Kaspar K.Mmuya ameongoza hafla ya chakula cha pamoja kwa watumishi wake,ambapo kama ilivyo ada, hafla hiyo imekwenda sambamba na kusherekea kumbukizi za siku za kuzaliwa kwa watumishi waliozaliwa mwezi Oktoba.Hafla hiyo imefanyika Leo tarehe 31 Oktoba 2024. Aidha katika hafla hiyo watumishi walipata mafunzo ya afya ya akili kutoka kwa msaikolojia wa Hospitali ya Taifa ya Akili (Mirembe) Bi.Gaudensia Kalalu. Msaikolojia kutoka Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe Bi.Gaudensia Kalalu, akitoa mafunzo kwa watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dodoma kuhusu namna mtu anavyoweza kuathirika na changamoto ya afya ya akili.  

RAS DODOMA ATEMBELEA MRADI WA JP-RWEE UNAOTEKELEZWA CHAMWINO

Image
Na. Hellen M. Minja,                   Habari – DODOMA RS Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya, ametembelea vikundi vya kina mama wajasiriamali wadogo pamoja na wakulima wanaowezeshwa na mashirika ya kimataifa kulima na kutengeneza bidhaa kitaalamu katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Oktoba 29,2024. Vikundi hivyo kutoka katika vijiji vya Chamwino Ikulu, Nayu na Dabalo vipo chini ya mradi unaojulikana kama JP-RWEE unaofadhiliwa na mashirika manne ya kimataifa ambayo ni FAO, IFAD, WFP na UN-WOMEN wenye lengo la kuboresha maisha ya wanawake waishio vijijini. Akiongea na wanawake walio kwenye mradi wa kuwezeshwa kupata hati miliki za ardhi katika kijiji cha Nayu, Kata ya Badalo, Bw. Mmuya ametoa wito kwa mashirika hayo kuwashirikisha wanawake hao kwenye kila wanachokifanya ili waweze kuwa na uelewa wa kutosha. “Shughuli zote za Serikali tunazozifanya, tuwaunganishe wananchi na Serikali yao wajue nini Serikali inawafanyia. Hi...

KAMPUNI YA OFFGRIDSUN YATAMBULISHA MRADI WA MAJIKO SANIFU NA BANIFU DODOMA

Image
Na. Hellen M. Minja,                 Habari – DODOMA RS Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule, leo Oktoba 29, 2024, ametembelewa na ugeni kutoka Kampuni ya OFFGRIDSUN ya nchini Italia katika ofisi yake iliyopo katika jengo la Mkapa Jijini Dodoma. Kampuni hiyo inayojishughulisha na usambazaji wa nishati jua (solar enegy) kwenye nchi za Kenya, Rwanda, Angola na Tanzania, kwa sasa imekuja na mradi mwingine mpya wa ‘Green Cook stove’ utengenezaji na usambazaji wa majiko sanifu na banifu yanayotumia nishati safi. Lengo la kumtembelea Mkuu wa Mkoa ni kutambulisha mradi huo unaotekelezwa kwenye mikoa mitatu hapa nchini ambayo ni Dodoma, Morogoro na Tanga. Mkoani hapa, mradi unatekelezwa kwenye Halmashauri mbili za Chamwino na Kongwa ambapo lengo ni kuzifikia kaya 23,000 za Chamwino na 26,000 za Kongwa. Akitoa ufafanuzi juu ya lengo la mradi huo hapa Dodoma, mwakilishi wa Kampuni hiyo nchini Bi. Valentina Quaranta, amesema; “Mradi unaleng...

ASKARI POLISI WA WILAYA YA DODOMA AKABIDHIWA PIKIPIKI

Image
Na Sofia Remmi  Habari-Dodoma Rs Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw.Kaspar K.Mmuya leo tarehe 28 Oktoba 2024,amekabidhi pikipiki moja kwa askari polisi wa Wilaya ya Dodoma kwa ajili ya kumuwezesha kutekeleza majukumu yake ya kutoa huduma na kufuatilia,kuzuia uhalifu na ukatili utakao jitokeza katika Wilaya hii. Kifaa hicho kimetolewa na Kituo Jumuishi kwa Manusura wa vitendo vya ukatili wa Kijinsia na ukatili dhidi ya watoto(One Stop Centre) kilichopo katika hospital ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma, ikiwa ni moja ya jitihada za kutokomeza ukatili wa Kijinsia Kituo hicho kinajumuisha Maafisa Ustawi wa Jamii,Madaktari,Wauguzi na Polisi, Huduma zinazotolewa katika kituo hicho jumuishi ni pamoja na kupokea na kushughulikia taarifa zote za ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto,kutoa huduma ya matibabu ikijumuisha uchunguzi wa ukatili aliofanyiwa Manusura,matibabu na majeraha,utoaji wa kinga dhidi ya VVU na uzazi wa mpango wa dharura kwa Manusura,kutoa ushauri nasaha na kuwalinda,kuelim...

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA

Image
Na Sofia Remmi  Habari-Dodoma Rs Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule ametembelewa na ugeni kutoka Baraza la Mitume na Manabii wa Mkoa Dodoma leo tarehe 28 Oktoba 2024. Lengo la ugeni huo ni kujitambulisha na kumjulisha juu ya mkutano mkubwa wa Kitaifa wenye lengo la Kuliombea Taifa utakaofanyika katika Mkoa wa Mwanza tarehe 11/11/2024. #kurayakosautiyako #dodomatupotayarikujiandikisha  #ujanjanikupigakura  #keroyakowajibuwangu  #dodomafahariyawatanzania  

KAMATI YA BUNGE TAMISEMI YATEMBELEA SOKO LA MACHINGA DODOMA

Image
Na. Hellen M. Minja,        Habari – DODOMA RS Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) leo Oktoba 28, 2024, imefanya ziara ya kikazi katika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na baadae  kukagua soko la wazi laWajasiriamali Wadogo (Machinga) lililojengwa katika kata ya Majengo, Mtaa wa Kitenge, tawi la Bahi Road. Kamati hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Justin L. Nyamoga pamoja na naibu waziri wa TAMISEMI Mhe. Festo Dugange, imetembelea na kujionea namna soko hilo lililojengwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu pamoja na mapato ya ndani ya Halamashauri ya Jiji la Dodoma linavyoendeshwa. Akizungumzia ukusanyaji wa ushuru wa soko kwa mwaka wa fedha 2023/2024 wakati akitoa taarifa ya uendeshaji wa soko hilo la wazi la Machinga, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Dkt. Frederick D. Sagamiko amesema; “kwa kipindi cha Julai, 2023/Juni 2024, soko la Machinga limeweza kukusanya kiasi cha shilingi Milioni 460 kati ya bilioni 1 iliyokisiwa, sawa n...

RC SENYAMULE ASHIRIKI UZINDUZI WA SOKO LA MWANAKWEREKWE ZANZIBAR

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule ameshiriki hafla ya uzinduzi wa Soko la Mwanakwerekwe lililopo katika Wilaya ya Magharib B” Visiwani Zanzibar tarehe 26 Oktoba, 2024. Mgeni Rasmi katika hafla hiyo alikua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ally  Mwinyi.  

WADAU WA KILIMO NA USTAWI WA JAMII WAKUTANA DODOMA

Image
Na. Siza Kangalawe,        Habari - DODOMA RS Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw.Kaspar Mmuya ameongoza kikao kazi cha wadau wa kilimo kutoka shirika lisilo la Kiserikali la 'Community Development Initiative Support  (CDIS)' lenye dhamira ya kujenga mabadiliko chanya na kuhakikisha ustawi wa jamii. Kikao hicho kimewajumuisha Seksheni ya kilimo ngazi ya Mkoa pamoja na Mkurugenzi wa CDIS Bw. Joseph Laizer  na timu yake,lengo likiwa  ni  kutambulisha mradi wa "Imarisha Fursa za Ajira kwa Vijana" ambao unaotarajia kufanyika kwa muda wa miezi 36 katika mikoa ya Dodoma na Morogoro ,ambapo bajeti ya Utekelezaji wa mradi huu kwa Mkoa wa Dodoma ni Dola za kimarekani 98,750,  kimefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Oktoba 25/2024.  

SEKRETARIETI YA MKOA WA DODOMA WAPIGWA MSASA.

Image
Na. Sizah Kangalawe Habari - RS Dodoma Menejimenti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma wakiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa huu Bw. Kaspar Mmuya, wamepatiwa mafunzo mbalimbali ya kiuongozi yanayolenga kuboresha utendaji kazi na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. Mafunzo hayo yamefanyika Oktoba 26,2024 katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hii, yakiwajumuisha Makatibu Tawala Wasaidizi  na Wakuu wa vitengo, ambapo katibu tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar Mmuya ametumia fursa hiyo kuwaagiza Viongozi hao kuyatumia maarifa waliyonayo kwa vitendo zaidi. "Niwaombeni tuu huko mbele tuendako myatoe maarifa mliyonayo na kuyaweka kwenye vitendo.Na ili mfanye, ni lazima muwe 'systematic'  kuendana na miongozo inayotakiwa, maana yake ni kutojitoa ufahamu na kufanya unavyotaka wewe.  Ni lazima ufuate muongozo,kwa sababu hicho unachotakiwa kufanya kinabebwa na cheo chako na sio jina lako", amesema Mmuya  Akizungumza wakati akitoa mafunzo hayo Mhadhiri Mwandamiz...

KILA LA HERI KIDATO CHA PILI

Image
 

MAONESHO YA MAUA YAZINDULIWA CHINANGALI PARK DODOMA

Image
Na. Hellen M. Minja,              Habari – DODOMA RS Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule, amezindua maonesho ya maua Mkoa wa Dodoma Oktoba 25, 2024, yanayowahusisha wanawake wa kikundi cha wanawake wauza maua Mkoani hapa wakishirikiana na wenzao kutoka mikoa ya Arusha, Dar Es Salaam na Kilimanjaro. Maonesho hayo ya siku tatu ambayo yameanza leo Oktoba 25 hadi Oktoba 27, 2024, katika viwanja vya Chinangali Park, yanalenga kukuza uelewa wa kutunza mazingira kwa kupanda miti na maua huku yakiongozwa na kauli mbiu ya “Panda maua na miti, pendezesha Dodoma” Akizindua maonesho hayo,Mkuu wa Mkoa, alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa wasimamizi wa majengo ya Serikali, kupanda  maua katika majengo hayo ili kupendezesha mandhari, lakini pia kupata hewa safi. “Nitoe wito kwa ofisi zote za Serikali Mkoa wa Dodoma, majengo yale yawe na oksijeni ya kutosha kwa kupanda maua, yawe na hewa ya kutosha na nzuri kwa kupanda maua, yawe na mvuto wa kut...

MAFUNZO YA UFUATILIAJI NA TATHMINI KWA WATUMISHI WA TAMISEMI YAFUNGWA RASMI

Image
Na Sofia Remmi.       Habari-Dodoma Rs. Katibu tawala mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya amefunga mafunzo ya ufuatiliaji na tathmini yanayoendeshwa na chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa watumishi waTawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa leo tarehe 25 Oktoba 2024. Mafunzo hayo ni sehemu ya mikakati ya serikali kuhakikisha maofisa hao wanasaidia kukamilisha mipango ya Serikali katika kupeleka shughuli za maendeleo kwa Wananchi kwa kuimarisha usimamizi, ufuatiliaji pamoja na tathmini ya maendeleo ya miradi inayotekelezwa na Serikali katika maeneo ya mamlaka hizo. Hii ni awamu ya kwanza kwa mafunzo hayo yaliyoanza Oktoba 21, 2024 na kumalizika leo Oktoba 25,2024,kufanyika katika mkoa huu, yakihusisha maafisa takriban 90 wanaosimamia vitengo vya ufuatiliaji na tathmini katika Halmashauri, Manispaa, Majiji na Mikoa kutoka katika mikoa 15 Nchini. #kurayakosautiyako #dodomatupotayarikupigakula #ujanjanikupigakura #mtiwangubirthdayyangu